member

Sunday 29 December 2013

Yerusalemu

Yerusalemu

Yerusalemu
Jerusalem Dome of the rock BW 13.JPG
Ukuta wa Maombolezo na Kuba ya Mwamba mjini Yerusalemu
Emblem of Jerusalem.svg
Seal
Flag of Jerusalem.svg
Flag
Jina laKiebraniaיְרוּשָׁלַיִם (Yerushalayim)
Jina laKiarabuالقـُدْس (al-quds);
rasmi: أورشليم القدس
(urshalim-al-quds)
Maana ya JinaKiebrania: "Urithi wa amani",
Kiarabu: "(Mji) mtakatifu"
UtawalaMji
Wilaya
Wakazi724,000 (Wayahudi 68%, Waislamu 30%, Wakristo 2%) (2006)
Eneo126,000  (126 km²)
MeyaNir Barkat
Tovuti rasmiwww.jerusalem.muni.il
Yerusalemu (mara kwa mara pia Kudisi) (kwa Kiebrania ירושלים Yerushalayim, kwa Kiarabu: القدس al-Quds) ni mji wa Mashariki ya Kati wenye pande mbili. Kwa upande mmoja ni mji mkuu wa Israel. Kwa upande mwingine Yerusalemu ya mashariki inatazamiwa kuwa mji mkuu wa Palestina ingawa imetawaliwa na Israel pia tangu 1967. Israel imetangaza tangu 1980 Yerusalemu yote kuwa mji wake mkuu wa milele, lakini nchi nyingi za dunia hazikubali azimio hili hivyo balozi za nchi za kigeni katika Israel ziko nje ya Yerusalemu.
Yerusalemu ina historia ndefu sana. Ni mji muhimu katika dini tatu zinazofuata imani ya Abrahamu, yaani UyahudiUkristo na Uislamu.
BlankAsia.pngMakala hii kuhusu maeneo ya Asia bado ni mbegu.
Je unajua kitu kuhusu Yerusalemu kama historia yake, biashara, taasisi zilizopo, watu au utamaduni?
Labda unaona habari katika wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

Saturday 21 December 2013

P FUNK

P. Funk

Paul Majani
P Funk Majani.jpg
Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwaPaul Matthysse
Pia anajulikana kamaP Funk, Majani, Kinywele Kimoja, Mdachi nk.
Asili yakeTanzania
Aina ya muzikiHip Hop na Bongo Flava
Kazi yakeMtayarishaji
AlaKinanda,Guitar, Kinakilishi
Miaka ya kazimn. 1995 -
StudioBongo Records
Ame/Wameshirikiana naMaster JayBonny Luv,Rajabu Marijani,Bizz Man, Boznia nk.
Paul Matthysse ( P Funk ) ni mtayarishaji wa muziki na pia mmiliki wa Studio ya Bongo Records iliyopo jijini Dar es SalaamTanzania. P Funk ambaye nusu Mtanzania nusu Mdachi, kama miaka ishirini iliyo pita hivi .P Funk a.k.a Majani, alikuwa na hisia za kupendelea muziki na pindi hadi kuamua kufanya kweli.. kuvutiwa kwake kupenda muziki ndio chanzo kikumbwa.. kilicho pelekea kufanikiwa vizuri katika muziki.
Kwenye Miaka 1991-92 wakati yupo bado shule IST (International School Of Tanganyika. Alikuwa mtundu mtundu kwenye studio za pale shule.. kupiga- piga midundo mbali mbali ya hapa na pale na kufoka-foka(Rap music) na pia alikuwa mbele sana kwa kupiga musiki kwenye Pati mbali mbali.. na hapo alikuwa kupenda sana musiki kwa ujumla.

Elimu ya Muziki na Uzoefu Wake[hariri]

P-Funk alikwenda kimasomo ya Mlio (sound) engineering kwa miezi 18 pale AmsterdamNetherland kabla ajaingia kwenye kutayarisha muziki. Alikuwa anajua kitu anachotaka kufanya. Mwaka 1995 akiwa na vifaa vyake vichache alianzisha kampuni yake ya kurekodi muziki nyumbani kwake. Na ni katika kipindi hicho hicho neno ’Bongo’lilipokuwa linatawala katika misemo ya kiswahili cha mitaani na lilikuwa linaelezea hali halisi ya maisha ya Dar es Salaam na ndio kipindi hicho album ya Bongo ilipozinduliwa. Akiwa bado ni mtayarishaji muziki mdogo, amefanikiwa kupata umaarufu mkubwa katika fani ya muziki na hasa katika milipuko ya nyimbo zenye ladha ya Bongo.
Anakubali kuwa amepata sana utaalam na mbinu kutokana na kufanya kazi watayarishaji wengine wa muziki wa Kitanzania kama Master J, Bonny Love na Rico. Mawazo yake na namna ya kuyaoainisha na muziki ndio hasa ambacho kinafanya muziki wake ufanikiwe.

Tuzo Alizopata[hariri]

Wasanii Aliowainua[hariri]

Kwanza alianza kwa kumpandisha chati Juma Nature ambaye ndio nyota wa nyimbo za Bongo Flava na akaendelea kwa kutayarisha santuri yaSolo ThangAYZay BSista PMike T na pia alishawahi kufanya kazi na Professor Jay alipotoa santuri yake mwenyewe. P Funk ana wasanii wengine wengi wanaotumia nembo ya kampuni yake katika Utengenezaji wa albamu.

Pia Anajulikana Kama[hariri]

  • P Funk
  • Halfani
  • Majani
  • Kinywele Kimoja
  • Mkono wa mungu
Musical notes.svgMakala hii kuhusu mwanamuziki fulani wa Afrika bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu P. Funk kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.
safi sana

Sunday 15 December 2013

HISTORIA YA George Washington

George Washington

Kutoka Wikipedia, kamusi elezo huru
Rukia: urambazaji, tafuta
Washington akisimamia shamba na watumwa.
Washington akivuka mto Delaware katika vita ya uhuru ya Marekani.
Sanamu ya Washington pamoja na maraisi wengine kwenye mlima Rushmore
Nyumba yake kwenye shamba la Mount Vernon
Washington kwenye pesa la Marekani.
George Washington (22 Februari 1732 hadi 14 Desemba 1799) alikuwa mwanasiasa, kiongozi wa kijeshi na rais wa kwanza wa Marekani kati ya 1789 na 1797.

Mtoto na kijana[hariri]

Alizaliwa kama mtoto wa pili wa mlowezi Augustine Washington katika koloni ya Virginia iliyokuwa mali ya mfalme wa Uingereza. Wazazi walikuwa na shamba kubwa lililolimwa na watumwa Waafrika. George alisoma shule miaka michache hakuendelea sana kielimu. Baada ya shule alianza kazi ya upimaji na ramani.

Mkulima na kiongozi wa kijeshi[hariri]

Baada ya kifo cha kakaye alirithi shamba kubwa pamoja na watumwa akawa mkulima mtajiri. Sehemu ya urithi ilikuwa cheo cha msimazi wa wanamgambo waliokuwa kikosi cha kijeshi cha hiari waliotakiwa kusaidiana na wanajeshi Waingereza kutetea koloni dhidi ya majirani Waindio na Wafaransa walioenea kuelekea kusini kutoka koloni yao ya Kanada - Quebec.
Katika umri mdogo wa miaka 22 Washington alijikuta kama mkuu wa wanamgambo katika vita ya Uingereza dhidi ya Wafaransa na Waindio iliyopanuka baada ye kuwa Vita ya Miaka Saba. Akaongoza kikosi chake dhidi ya maadui akafaulu mara kadhaa. Baadaye alishirikiana na jeshi rasmi la Uingereza katika mapigano ya Monongahela na kuongoza mabaki ya jeshi baada ya kifo cha jemadari Mwingereza. 1755 akawa mkuu wa jeshi la koloni Virginia. Lakini baada ya ushindi Waingereza walikataa kumpa cheo katika jeshi la mfalme hivyo akajiuzulu akirudi kwa shamba lake na kufuata siasa kwenye bunge la koloni.
1759 Washington akamwoa mjane mtajiri akawa kati ya matajiri kabisa wa Virginia.

Mapinduzi[hariri]

Baada ya vita ya miaka saba uhusiano kati ya Uingereza na walowezi Waingereza katika koloni zake 13 za Amerika ya Kaskazini ukazorota. Tangu 1773 Waingereza walitumia sheria ya dharura na nguvu ya kijeshi mjini Boston. Wawakilishi wa koloni zote 13 wakakutana kama bunge la Amerika Bara na Washington alikuwa miongoni mwao.
Baada ya mapigano ya kwanza kati ya wanajeshi Waingereza na wanamgambo wa walowezi bunge likaamua kuunda jeshi la pamoja la koloni zote na Washington akateuliwa kuwa jemadari mkuu.
Aliongoza jeshi la Marekani katika vita ya uhuru wa Marekani dhidi ya Uingereza hadi mwaka 1783.

Baada ya vita: mwanasiasa na rais[hariri]

Baada ya vita ya uhuru ya Marekani Geroge Washington akarudi kwake akalima tena lakini akachaguliwa pia kama mwakilishi wa Virginia katika bunge la katiba la Marekani mwaka 1787 akawa mwenyekiti wa mkutano huu uliokubali katiba ya Marekani.
4 Februari 1789 alichaguliwa kuwa rais wa kwanza wa Marekani akirudishwa mwaka 1789. Baada ya kipindi chake cha pili alikataa kusimama tena akaunda hivyo utaratibu ya kwamba rais anaweza kurudishwa mara moja tu hawezi kuendelea zaidi.

Uzee[hariri]

1797 akarudi tena kwake shambani aliposimamia kilimo kilichoendeshwa na watumwa 390. Tar. 14 Desemba alikufa kwake nyumbani. Kabla ya kuaga dunia aliamuru katika usia wake ya kwamba watumwa wake wote warudishiwe uhuru baada ya kifo chake yeye mwenyewe na mke wake.
Mji mkuu wa Marekani Washington, D.C. na jimbo la Washington vimepokwa majina kutokana naye. Picha yake iko kwenye noti ya dollar moja.

Sunday 8 December 2013

Juma Nature

Juma Nature

Juma Nature
Juma Nature
Juma Nature
Maelezo ya awali
Jina la kuzaliwaJuma Kassim Ally
Pia anajulikana kamaSir. Nature
Kibla
Msitu wa Vina
Jitu la Maneno ya Shombo
Amezaliwa1980
Kazi yakeRapa
Miaka ya kazi1997 - hadi leo
StudioBongo Records
Sound Crafters Records
Mj Records
Ame/Wameshirikiana naDknob
Mh Temba
Dark Master
TID
Solo Thang
Professor Jay
AY
Inspector Haroun
Chegge
Mandojo na Domokaya
Zay B.
Juma Nature au Sir Nature (amezaliwa mwaka 1980 kama Juma Kassim Mohamed Kiroboto jijini Dar es Salaam) ni mwanamuziki wa kizazi kipya maarufu kama Bongo Flava kutoka nchi ya Tanzania. Pia ni muanzilishi wa kundi la Tmk Wanaume.
Nature ni msanii mbunifu katika Bongo Flava na Hip Hop ya kiTanzania. Sio mtunzi tu pia ana kipaji cha kujaliwa na sauti nzuri ya uimbaji. Sababu nyingine zipelekeazo muziki wa Juma Nature upendwe Afrika Mashariki ni mashairi anayotunga. Baadhi za nyimbo zilizompa heshima kitaifa ni ile ya 'Umoja wa Tanzania' ambayo yenyewe ilikuwa inataka kupatanisha mgogoro wa kisiasa kati ya vyama vya CCM na CUF. Hakuishia hapo, zipo nyimbo nyingine nyingi tu zenye kutoa husia kwa Taifa.
Nature ni mmoja bora, vema anajulikana na wengi katika ubunifu wasanii Bongo Flava Kiswahili hip hop genre, si tu ndiye mtunzi kubwa na ya kipekee rap talented artist lakini pia vipawa na kugusa soulful na sauti. Albamu yake Mpya, "Bongo Flava: Swahili Rap from Tanzania", wengi lyrics ambayo ni tracks yake sasa ni pamoja na matatizo ndani ya nchi yake. Baadhi ya matatizo yeye raps kuhusu pamoja, "VVU / UKIMWI, mkutano ugumu wa mahitaji ya msingi, darasa na mali vizuizi, na kufanya kichwa yako high licha ya kila kitu" [1] Mmoja wa Nature's vizuri kända nyimbo ni "Umoja wa Tanzania" ambayo mazungumzo kuhusu maadhimisho ndani ya Tanzania na hisia ya umoja kuwa lina exemplified [1] "Utajiju" ( "it's up to you") kutoka Juma Nature's brand new albamu Ubin-Adam Kazi, ni wimbo kuhusu watu walio kama wao noses ndani poke wengine 'biashara [2]
Sababu kuu nyingine umaarufu wake kote Afrika Mashariki ni wa kozi mada nyimbo yake, ambayo kwa kweli na kushughulikia masuala relevanta wengi wa watu mtaa.[onesha uthibitisho] "Umoja wa Watanzania" kutoka Ugali albamu yake ya 2004, kwa mfano, akipatikana kwa amani azimio kutoelewana kisiasa baina ya vyama viwili Rival, chama tawala cha CCM na CUF, kuwakumbusha watu wa nini inaweza kuwa matokeo ya mgogoro wa kisiasa.
Wanaume Family ni kitengo wasanii tofauti yaani Juma Nature, Wachuja Nafaka, GWM / Gangsters na matatizo (Matatizo), Wangoto Family, naGangwe Mobb. Wanaume Family maendeleo kwa lengo la kubadilishana mawazo juu ya jinsi ya kutumia Kiswahili hip hop positively, kitaifa na kimataifa, kukuza na kutumia umoja wao kama njia ya kusaidia wasanii wengine ujao.
Hisia zao ni togetherness mara nyingi kuonekana katika prestanda yao moja kwa ubunifu wao line "mapanga Shwaaa! Shwaaaa! " ngoma ambayo anatoa mashabiki kwa karibu Frenzy. Na wao wakicheza mtindo wa kipekee, kwamba wa mateke high na kuruka juu na chini na anafanya shingo ngoma, ni tu breathtaking. Hakuna ajabu wao sasa kupata walioalikwa kutumbuiza mbele ya wasomi watazamaji. Kundi ya Wanaume Family kupasuliwa mwezi Novemba 2006. Nature kuweka pamoja kundi mpya chini ya jina la Wanaume Halisi, Luteni akimshirikisha kalama, Dollo, Richie One, Bob Q, BK, D Chief, A Man, kakaman, Maripo, Mzimu, Eddo na Inspekta Haroun.

Albamu Alizotoa[hariri]

  • Nini Chanzo (2001)
  • Ugali (2003)
  • Ubinadamu-Kazi (2005)
  • Zote History (2006)
Musical notes.svgMakala hii kuhusu mwanamuziki fulani wa Afrika bado ni mbegu.
Je, unajua kitu kuhusu Juma Nature kama wasifu wake, habari za maisha au kazi yake?
Labda unaona habari katika Wikipedia ya Kiingereza au lugha nyingine zinazofaa kutafsiriwa?
Basi unaweza kuisaidia Wikipedia kwa kuihariri na kuongeza habari.

References[hariri]

Friday 6 December 2013

Benjamin Mkapa

Benjamin Mkapa

Rukia: urambazaji, tafuta
Benjamin Mkapa

Muda wa Utawala
23 November 1995 – 21 December 2005
Makamu wa Rais Omar Ali Juma (1995–2001)
Ali Mohamed Shein (2001-05)
mtangulizi Ali Hassan Mwinyi
aliyemfuata Jakaya Kikwete

Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu,
Muda wa Utawala
1992 – 1995
Rais Ali Hassan Mwinyi

Waziri wa Habari na Utangazaji
Muda wa Utawala
1990 – 1992
Rais Ali Hassan Mwinyi

tarehe ya kuzaliwa 12 Novemba 1938 (umri 75)
Ndanda, Masasi, Tanganyika
utaifa Mtanzania
chama
ndoa Anna Mkapa
watoto 2
mhitimu wa Chuo Kikuu cha Makerere
Chuo Kikuu cha Columbia
Fani yake mwandishi wa habari, mwanadiplomasia
dini Ukristo
Benjamini William Mkapa (amezaliwa 12 Novemba 1938) ni Rais wa zamani wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania (1995-2005) na Mwenyekiti wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi, CCM (Revolutionary State Party).[1]

Wasifu

Mkapa ni mhitimu wa Chuo Kikuu cha Makerere.[1] Nafasi alizoshikilia zamani ni pamoja na kuwa afisa wa utawala huko Dodoma na Waziri wa Sayansi, Teknolojia na Elimu ya Juu. Yeye pia aliongoza ujumbe wa Tanzania huko Marekani na alikuwa Waziri wa Mambo ya Nje kutoka 1977 hadi 1980 na kutoka 1984 hadi 1990.[2]
Katika mwaka wa 1995, Mkapa alichaguliwa rais msingi wake ukiwa kwa kampeni maarufu ya kupambana na ufisadi na kwa kumuunga mkono kwa nguvu rais wa zamani Julius Nyerere [3] Juhudi za Mkapa za kupambana na ufisadi ni pamoja na kuumba jukwaa la wazi lililoitwa Tume ya Rais juu ya Ufisadi (Tume ya Warioba) na kuongeza msaada kwa Afisi ya Kuzuia Ufisadi.[3]
Muhula wa pili wa miaka 5 wa Mkapa kama Rais uliisha Desemba 2005. Katika wakati wake ofisini, Mkapa alibinafsisha makampuni yanayomilikiwa na serikali na akaweka sera za soko huru.[4] Wafuasi wake walimtetea kuwa kuvutia uwekezaji wa kigeni ungesaidia kukuza uchumi. Sera zake zilipata msaada wa Benki ya Dunia na IMF na kupelekea baadhi ya madeni ya nje ya Tanzania kufutiliwa mbali.[3]
Amekashifiwa kwa upungufu wa baadhi ya jitihada zake za kupambana na ufisadi [3] vilevile njia yake duni ya kutumia fedha. Alitumia £15 milioni kununua ndege ya kibinafsi ya kirais, vilevile karibu £30 milioni kwa vifaa vya angani vya kijeshi ambavyo wataalam waliona yalizidi mahitaji machache ya majeshi ya nchi .[5] Ilikuwa juu ya ununuzi huu wa mwisho ndipo Katibu wa Maendeleo ya Kimataifa wa Uingereza wa wakati huo Clare Short alielezea hasira ya umma, na kusababisha yeye kujulikana kama 'Mama Radar' katika vyombo vya habari vya Tanzania.
Baada ya kutoka ofisini kutokana na kukamilisha mihula miwili inayoruhusiwa, Mkapa anakumbwa na shutuma nyingi za ufisadi kati yao kujipa mwenyewe na Waziri wake wa zamani wa nishati na madini Daniel Yona "Mgodi wa Makaa ya Mawe wa Kiwira" yenye faida kubwa katika Nyanda za juu za kusini mwa Tanzania bila taratibu zifuatazo. Kwa kujibinafsishia mwenyewe mgodi wa makaa ya mawe wa Kiwira, alivunja katiba ya Tanzania ambayo haimruhusu rais kufanya biashara yoyote katika ikulu.
Aliteuliwa katika Bodi ya Wadhamini ya Chuo cha Aga Khan mwezi Novemba 2007.[4]

Heshima na Tuzo

Nishani

Nishani Nchi Mwaka Ref
Order of the Golden Heart of Kenya.svg Nishani ya Moyo wa Dhahabu wa Kenya (Chifu) Bendera ya Kenya Kenya 2005 [6]
Order of Mwalimu Julius Kambarage Nyerere (Tanzania) - ribbon bar.png Nishani ya Mwalimu Julius Kambarage Nyerere Bendera ya Tanzania Tanzania 2011

Shahada za Heshima

Chuo Kikuu Nchi Shahada ya Uzamivu Mwaka Ref
Chuo Kikuu cha Sōka Bendera ya Japani Japan Shahada ya Heshima 1998 [7]
Chuo cha Morehouse Flag of the United States.svg Marekani Shahada ya Heshima 1999 [7]
Chuo Kikuu Huria cha Tanzania Bendera ya Tanzania Tanzania Shahada ya Heshima 2003 [7]
Chuo Kikuu ya Kitaifa cha Lesotho Bendera ya Lesotho Lesotho Daktari wa Sheria 2005 [7]
Chuo Kikuu cha Kenyatta Bendera ya Kenya Kenya Daktari wa Elimu 2005 [8]
Chuo Kikuu cha Dar es Salaam Bendera ya Tanzania Tanzania Shahada ya Heshima 2005 [7]
Chuo Kikuu cha Nyukasal Flag of the United Kingdom.svg Uingereza Daktari wa Sheria ya Kiraia 2007 [9]
Chuo Kikuu cha Rasi ya Pwani (Cape Coast) Bendera ya Ghana Ghana Daktari wa Barua 2008 [10]
Chuo Kikuu cha Makerere Bendera ya Uganda Uganda Daktari wa Sheria 2009 [11]

Marejeo

  1. Jump up to: 1.0 1.1 [1] ^ "Benjamin Mkapa", Microsoft Encarta Encyclopedia 2001, WGBH (FM), pbs.org, ilitolewa 19-Oktoba-2009
  2. Jump up Benjamin Mkapa,
  3. Jump up to: 3.0 3.1 3.2 3.3 [4] ^ Bruce Heilman na Laurean Ndumbaro, "Corruption, Politics and Societal Values in Tanzania: An Evaluation of the Mkapa Administration's Anti-Corruption Efforts", Afr. J. polit. sd. (2002), Toleo 1 Nambari 7
  4. Jump up to: 4.0 4.1 [10] ^ "Mheshimiwa Benjamin William Mkapa", Bodi ya Wadhamini, Chuo cha AKU, ilitolewa 19-10-2009
  5. Jump up [9] ^ Gideoni Burrows, "We sell arms to Saddam's friends", New Statesman, 8 Septemba 2003
  6. Jump up Mkapa lauds Kenya's democratic posture. panapress.com (12 October 2005). Rudishwa juu ya 26 Septemba 2013.
  7. Jump up to: 7.0 7.1 7.2 7.3 7.4 83RD Annual District Conference & Assembly (PDF) (Kiingereza). Page 10, Rotary International District 9200 (17 May 2008). Rudishwa juu ya 26 Septemba 2013.
  8. Jump up Prominent Alumni (Kiingereza). Kenyatta University. Rudishwa juu ya 26 Septemba 2013.
  9. Jump up Citation: Benjamin William Mkapa DCL (PDF) (Kiingereza). Newcastle University (2007). Rudishwa juu ya 26 Septemba 2013.
  10. Jump up UCC honours former Tanzanian leader (Kiingereza). Rudishwa juu ya 26 Septemba 2013.
  11. Jump up H.E. Benjamin Mkapa receives Makerere Honorary PhD (Kiingereza). Makerere University (27 November 2009). Rudishwa juu ya 26 Septemba 2013.

Viungo vya nje

Alitanguliwa na
Ali Hassan Mwinyi
Rais wa Tanzania
1995-2005
Akafuatiwa na
Jakaya Kikwete
Kigezo:Tume kwa Afrika

Viungo vya nje

Wikiquote-logo.svg
Wikiquote ina mkusanyiko wa dondoo kuhusu: